MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

TANZANIA  KUSIMAMIA WANAJESHI WA PAMOJA DRC
Picha ya Rais wa Tanzania ambaye ni mwenyekiti wa SADC

Jumla ya nchi kumi katika eneo la Maziwa makuu zimekubaliana kuunda jeshi la pamoja litakalokuwa na jumla ya askari 4,000 katika kukabiliana na ghasia na vita vya mara kwa mara mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Raiya wa DRC wakiwa mitaani na watoto wadogo wakiangaika kutokana na machafuko nchini humo
 Waziri wa Ulinzi wa DR Congo, Dakta Crispus Kiyonga amethibitisha uundwaji wa jeshi hilo, akisema litafanya kazi chini ya usimamizi wa Tanzania.
Mapigano ya hivi sasa mashariki mwa Congo yalizuka mwezi Aprili mwaka huu wakati waasi wa M23 walipoliasi jeshi la nchi hiyo na kusababisha watu laki tano kuyakimbia makaazi yao wakihofia usalama wao.
Wakati huohuo, viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika, SADC, wameanza mkutano wao wa dharura jijini Dar es salaam nchini Tanzania.
Wameanza kwa kufanya kikao cha Asasi ya Ulinzi, Siasa na Usalama ya SADC inayojulikana kama TROIKA chini ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania.

Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment