MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

WAANDAMANAJI 10 WAUWAWA NA WANAJESHI 
Baadhi ya Wanajeshi wa Sudani Kusini wakiwa na zana za kijeshi
Umoja wa Mataifa unasema kuwa jeshi la Sudan Kusini limewapiga risasi na kuwauwa watu 10, ambao walikuwa wakiandamana kupinga kuhamishwa kwa makao makuu ya serikali za mitaa magharibi mwa nchi.
Afisa wa kuweka amani wa Umoja wa Mataifa huko Bahr el-Ghazal amesema watu wane waliuwawa katika mji wa Wau kwenye mapambano ya jana usiku.
Na wengine sita waliuwawa baada ya kukusanyika kulalamika juu ya mauaji ya awali.
Jeshi la Sudan Kusini limekataa kusema kitu.

Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment