MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

RAIS KAGAME APEWA ONYO
Rais Barrack Obama wa Marekani ametoa wito kwa rais wa Rwanda Paul Kagame, kusitisha msaada anaotoa kwa makundi ya waasi nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Raisi wa marekan Barrak Obama
 Kwa mujibu wa ikulu ya White House, rais Obama alifanya mazungumzo ya simu ya Rais Paul Kagame siku ya jumanne, ambapo aliafiki tangazo lake la kujitolea katika harakati za kupatikana kwa amani katika Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Waasi wa M-23 wapo katika eneo la mashariki mwa Congo licha ya kuwepo kwa wanajeshi wa kutunza amani wa umoja wa mataifa katika eneo hilo.
Ripoti ya hivi majuzi iliyochapishwa na Umoja wa Mataifa iliishutumu serikali ya Rwanda kwa kutoa msaada kwa waasi hao wa Congo, madai ambayo serikali ya Rwanda Imekanusha vikali.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment