MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

NAY WA MITEGO, OSTAZ JUMA AMENIKOSEA SANA KUPITA ALIVYOMKOSEA PNC



 Nay wa Mitego: Katika watu waliowahi kunikosea Ostaz Juma amenikosea kupita maelezo, kuliko PNC
Msanii wa Hip Hop nchini Tanzania Nay wa Mitego, amefunguka na kusema kupitia kipindi cha  Bongo Dot Home ya 100.5 Times Fm kuwa kitendo alichokifanya Ostaz Juma kupost picha zinazomuoenesha PNC akimpigia magoti, kwa upande wake amemkosea yeye hata kuliko PNC mwenyewe.”............


“kumpigia mtu magoti kwa ajili ya kuomba msamaha ni sahihi. Lakini kuna upigiaji wa magoti mwingine ambao baadae unaweza kuonesha picha mbaya kuwa umedhamilia kumdhalilisha. Halafu Ostaz Juma hana nidhamu halafu ni mtu ambaye hajitambui. Vijisenti anavyovipata nadhani ndivyo vinampa jeuri ya kudhalilisha wasanii wenzetu, sio kitu kizuri.


Mimi tangu nilipoona hizo picha nilisema siwezi kumpenda hata siku moja, hata salamu yangu siwezi kumpa. Siwezi kumheshimu hata kidogo. Nitamdharau kuliko kitu chochote, kuliko mtu yeyote aliyewahi kunikosea sana. Ila katika watu ambao waliowahi kunikosea, nafikiri mimi Ostaz Juma amenikosea kupita maelezo. Kuliko alivyomkosea PNC mwenyewe.”

Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment