Rais
mpya wa Sri
Lanka Maithripala Sirisena anatarajiwa kuapishwa baadaye leo.
Hatua
hiyo inakuja baada ya Rais anayemaliza muda wake, Mahinda Rajapaksa kukubali
kushindwa katika uchaguzi mkuu uliofanyika Alhamisi............
Amekubaliana
na ushindi alioupata mpinzani wake katika uchaguzi huo. Kiongoazi huyo mpya
Maithripala Sirisena aliwahi kuwa waziri katika serikali ya nchi hiyo.
Msemaji
wa Rais wa Sri Lanka amesema Bwana Rajapaksa ameondoka katika makaazi ya Rais
na atahakikisha anayakabidhi madaraka kiutaratibu.
Baada
ya kutangazwa kushindwa kwa Rajapaksa fataki zilipigwa maeneo mengi ya nchi .
Aliitisha uchaguzi mapema kwa matumaini ya kulinda nafasi yake ya kukaa
madarakani kwa awamu ya tatu.
chanzo BBC
0 maoni:
Post a Comment