Mshirikishe mwenzako
AFP
Aliyekuwa kiongozi kwa muda mrefu nchini Cuban Fidel Castro amewashukuru wafuasi wake kwa kumtakia heri akitimiza umri wa miaka 90.
Kwenye barua iliyochapishwa kwenye gazeti la chama tawala cha kikomunisti nchini humo, amesimulia kumbukumbu za maisha yake ya ujana.
Baadaye, amezisifu Uchina na Urusi lakini akamshutumu Rais wa Marekani Barack Obama.
Fidel Castro alitawala Cuba kwa zaidi ya miaka hamsini kabla ya kumkabidhi nduguye Raul madaraka.
Raul Castro ameleza mengi ya masharti ya kiuchumi yaliyokuwa yamewekwa chini ya utawala wa Fidel na pia akafufua uhusiano na Marekani.
0 maoni:
Post a Comment