MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

Shambulio la bomu laua watu 30 harusini Uturuki

Shambulio la bomu lililoilenga sherehe ya harusi iliyokuwa ikifanyika nje, kusini mashariki mwa Uturuki, limesababisha vifo vya zaidi ya watu 30 na wengine 94 kujeruhiwa Jumamosi hii.
TURKEY1-master768
Naibu Waziri Mkuu, Mehmet Simsek, alisema kuwa shambulio hilo lililotokea kwenye mji wa Gaziantep, karibu na mpaka wa Syria, limeonekana kusababishwa na mtu aliyejitoa mhanga. Maafisa wengine wanadai kuwa shambulio hilo linaweza kuwa limefanywa na wanamgambo wa kikurdi au kundi la Islamic State, ISIS.
Picha zilizopigwa baada ya mlipuko huo, zimeonesha miili kadhaa ikiwa imefunikwa na mashuka maupe.
Hivi karibuni Uturuki imekuwa ikikumbwa na mashambulio ya kigaidi. June, watu waliokuwa na silaha na mabomu walishambulia uwanja wa ndege wa mji mkuu, Istanbul na kuua zaidi ya watu 40.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment