MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

MWISHO MWAMPAMBA AFANYIWA UNYAMA WA UBAGUZI NCHINI NAMIBIA

Mshiriki wa BBA, kipindi cha miaka kadhaa iliyopita, Mwisho Mwampamba, ambaye kwa sasa anaishi nchini Namibia, amefunguka kupitia Facebook, na kusema kuwa Namibia ni nchi inayofanya ubaguzi wa hali ya juu kabisa.

Mwisho aliandika maneno haya yenye simanzi kubwa sana kwa kila Mtanzania, na kitu kinachopelekea baadhi ya Watanzania kuichukia Namibia na Afrika Kusini kwa kutufanyia Ubaguzi ingawaje wote ni mablack. ( kwakuwa Namibia Ipo HURU, naona woga dhidi ya raia wa kigeni (xenophobia) imekuja kwa kasi. P;lisi walikuja nyumbani kwangu na kuniambia natakiwa nirudi kwenye nchi yangu, manyanyaso kwenye mpaka, Huwa Napata Visa ya Miezi miwili tu, licha ya kuwa SADC na nimeoa Mnamibia, Swali langu ni , Mveterani wenu wote wametoka wapi ? Mnawatendea wakoloni wenu wa zamani vizuri kuliko wakombozi wenu ? Huwa inafedhehesha kuona jinsi Wanamibia na waafrika kusini walivyo.

Wanamibia na waafrika Kusini wanatutendea sisi waafrika wengine kama nyani kwakuwa sasa mko huru. Wamesahau mapema jinsi tulivyowasaidia  japokuwa masikini na wenye njaa, ni sawa tulifanya sababu kilikuwa ni kitu sahihi kufanya na sikupata fadhila yenu, lakini tunatarajia walau heshima na kutendewa kama Binadam) Hayo yalikuwa maneno ya mwisho, maneno yanatia uchungu sana na kuona jinsi gani Watanzania Tunavyofanya ingawaje tumejawa na roho njema.


Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment