MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

RAIS KIKWETE” TANZANIA HATUJITOI AFRIKA MASHARIKI


Rais wa Tanzania , J.M. Kikwete

Tanzania imesema hataitajitoa katika Jumuiya ya Afrika kama wengi walivyodhani na badala yake imedhamiria kuhakikisha Jumuiya hiyo inadumu na kustawi.

Akilihutubia bunge la Tanzania, mjini Dodoma, katikati mwa Tanzania, Rais wa nchi hiyo, Jakaya Kikwete amesema kwamba Tanzania haina mpango wala fikra za kujitoa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuwa ni nchi inayoamini katika umoja na maendeleo na imekuwa ikitumia gharama kubwa kuhakikisha jumuiya hiyo inaimarika.

"Tanzania ni mwanachama mvumilivu, mtiifu na mwaminifu na tunatimiza wajibu wetu kwa jumuiya na kuhusika kikamilifu katika ujenzi wake." amesema Rais Kikwete.

Rais Kikwete ametumia muda mrefu katika hotuba hiyo kuchambua masuala mbalimbali ya msingi ya uhai wa jumuiya hiyo huku akisema ameshangazwa na nchi za Kenya, Uganda na Rwanda kuzitenga Tanzania na Burundi.

Amesema kuna masuala ambayo hayazifungi nchi wanachama katika mkataba wa umoja wao, hivyo kuwa na uhuru wa ushirikiano na nchi ndani ya jumuiya na hata nje.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment