AJALI YA NDEGE YAUA WATU 77, NA MMOJA TU KUKUTWA BADO YUHAI.
Ndege ya kijeshi aina ya Hercules C-130 ya Algeria ilikuwa na familia za wanajeshi wakielekea mji wa Costantine lakini ilipofika kwenye milima ya Oum al-Bouaghi kutokana na hali mbaya ya hewa ikapata ajali na kusababisha vifo vya watu 77 kati ya 78 waliokuwa katika ndege hiyo.........
Taarifa za mwanzo zilisema kuwa ndege hiyo ilbeba watu 103, maafisa wa ulinzi walisema kuwa ndege hiyo ilibeba watu 78 na waliokufa ni 77, mmoja tu ndio yuko hai na anaendelea na matibabu hospital.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na wizara ya ulinzi imesema kuwa hali mbaya ya anga iliyohusisha kimbunga na mvua kubwa ya barafu ilisababisha ajali hiyo.
0 maoni:
Post a Comment