Uamuzi wa bodi ya
Filamu Tanzania (TFB)
kuizuia filamu ya muigizaji wa kiume na mkongwe, Dk Cheni ‘Nimekubali Kuolewa’,
kwa madai ya kukiuka maadili na kuchochea tabia za ushoga, umepingwa na msanii
huyo ambaye anaamini kabisa kuwa maudhui ya filamu hiyo yangeelisha jamii zaidi
ya picha katika cover yake.
Hapa alifunguka alipokuwa akiiambia Global Publisher “Eti
ushoga wangu uko kwenye kujiremba sana,
wamenionea, lengo letu ni kukemea na kupinga vikali vitendo vya ushoga na ndoa
za jinsia moja, huwezi kuelimisha bila kuonesha madhara yake kwa vitendo kama ilivyo kwenye filamu hiyo. Amesema Dk Cheni.
Kupitia Tovuti ya Times fm, alifunguka na kusema kuwa
“Nahisi filamu inayokuja inaitwa ‘Nimekubali Kuolewa’, itakuwa ya kipekee
sana, kwa sababu hata pale kwenye cover lake tu itakuwa ‘unique’ kwa sababu
ntakuwa nimekaa nimevalishwa shela, kuonesha kwamba ni kweli nimekubali
kuolewa, hii itakuwa tofauti na movie nyingi nilizowahi kucheza, itakuwa
‘Unique’.” Dk Cheni aliiambia tovuti ya Times Fm.
0 maoni:
Post a Comment