Mamlaka nchini Sierra Leone imeanza
kutekeleza hatua ya kutotoka kwa siku tatu miongoni mwa raia wake itakayosaidia
kukabiliana na kuenea kwa mlipuko wa ugonjwa wa ebola.................
Takriban
watu millioni sita wametakiwa kusalia majumbani mwao kwa kipindi cha siku tatu
huku watu wa kujitolea wakitembelea nyumba hadi nyumba kuwasaka watu walio na
ishara za ugonjwa huo huku wakiwashauri wengine jinsi ya kuepuka maambukizi.
Visa
kadhaa bado vinaendelea kuripotiwa kazkazini na Magharibi mwa Sierra Leone kila
wiki.
Mataifa
matatu ya Afrika Magharibi yalioathiriwa vibaya na Ebola Sierra
Leone,Liberia,Guinea-yameweka lengo la kutokuwa na hata kisa kimoja cha ebola
ifikiapo katikati ya mwezi ujao.
Kutoka
BBC Swahili.
0 maoni:
Post a Comment