Waziri
mkuu mwanzilishi wa Singapore, Lee Kuan Yew amefariki dunia.
Lee
amefariki akiwa na umri wa miaka tisini na mmoja kutokana na ugonjwa wa mapafu......................
Kwa
miongo mitatu ya utawala wa Lee alifanikiwa kuipitisha nchi yake katika kipindi
cha mpito na kuleta mabadiliko makubwa
ya
kiuchumi hasa katika usafirishaji majini kwa kutumia rasilimali kidogo
walizokuwa nazo na sasa kuwa kitovu kikubwa cha kibiashara cha kimataifa.
David
Adelman ni balozi wa zamani wa Marekani nchini humo, ametuma salamu zake za
rambi rambi.
Kifo
cha Lee ni mwisho wa enzi zake.
mwisho
wa mwanamume mwenye nguvu ya ushawishi aliyeingia madarakani katikati ya miaka
ya sitini .
Lee
alifanikiwa kuanzisha ushirikiano wa kirafiki kati ya nchi yake na Marekani
ambao umedumu hata leo
na
unaweza kuvuka mipaka sio kwa singapore tu bali hata kwa watu wa Asia ya kusini
Mashariki.
Viongozi
mbalimbali duniani wanaendelea kutuma risala za rambirambi kwa Singapore, baada
ya kifo cha Lee Kuan Yew hospitalini.
Yew
aliaga dunia akiwa na umri wa miaka 91 baada ya kuugua homa ya mapafu.
Nchini
Uchina, wizara ya mashauri ya nchi za kigeni imemsifia na kumtaja Lee Kuan Yew,
kama kiongozi wa kipekee wa bara Asia.
Marehemu
Lee ambaye aliiletea mabadiliko makubwa taifa la Singapore na kuwa na mojawepo
ya bandari maarufu zaidi Duniani huku uchumi wa nchi hiyo ukiimarika maradufu,
atasalia katika kumbukumbu la taifa hilo.
Mwanawe
ambaye ni waziri mkuu wa sasa nchini humo, Lee Hsien Loong, anasema kuwa
Singapore haitawahi kuwa na mtu kama huyo tena.
Katika
risala zake za rambirambi, Rais Barrack Obama wa Marekani amemtaja kama gwiji
wa historia.
Nchini
Uchina, wizara ya mashauri ya nchi za kigeni imemsifia na kumtaja Lee Kuan Yew,
kama kiongozi wa kipekee wa bara Asia.
Naye
waziri mkuu wa Uingereza, David Cameron, anasema kuwa Bwana Lee alikuwa
mmojawepo wa viongozi wakuu duniani.
Serikali
ya Singapore imetangaza siku sita ya maombolezo, hadi atakapozikwa siku ya
Jumapili.
kutoka BBC Swahili.
0 maoni:
Post a Comment