Ndege
za kijeshi za Kenya zimeshambulia maeneo ya wapiganaji wa kundi la Alshabaab
katika taifa jirani la Somalia ,msemaji wa jeshi ameiambia BBC........
Ndege
hizo zililenga maeneo mawili ya jimbo la Gedo,linalotumiwa na wapiganaji hao
kuvuka na kuingia Kenya, msemaji huyo ameongeza.
Maeneo
hayo mawili hutumiwa na wapiganaji hao kupanga mshambulizi nchini Kenya.
Wanajeshi
wa AMISOM walitarajiwa kupeleka wanajeshi wao katika eneo hilo la Gedo lakini
hadi sasa hawajafanya hivyo.
Hili
ni shambulio la kwanza la Kenya kwa shambulizi la alshabaab ambalo lilisababisha
mauaji ya watu 148 katika chuo kikuu cha Garissa wiki iliopita.
Rais
wa Kenya Uhuru Kenyatta ameapa kujibu shambulizi hilo kwa njia mbaya zaidi.
Msemaji
wa jeshi la Kenya David Obonyo ameiambia BBC kwamba Jeshi la Kenya lilijibu
vitisho kwa kutekeleza mashambulizi ya angani siku ya jumapili usiku katika
eneo hilo.
Hakuna maelezo zaidi ya oparesheni hiyo yaliotolewa
kutoka BBC Swahili
0 maoni:
Post a Comment