MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

WATU 25 WAUAWA " R.I.P"

Maafisa wa serikali Kaskazini mwa Nigeria wamesema kuwa watu 25 wameuawa katika shambulio la bomu la kujitolea mhanga katika mji wa Zaria...........


Ripoti zinasema kuwa watu wengine 32 wamejeruhiwa kwenye shambulizi hilo.
Shambulio hilo lilitokea katika jengo moja la serikali ambako wafanyakazi wa serikali walikuwa wamekusanyika kusajiliwa.

Wengi waliokuweko ni walimu na wafanyikazi wa umma.
Katika kipindi cha majuma 2 yaliopita takriban watu 220 wameuawa katika mashambulizi kadha yanayolaumiwa kutekelezwa na kundi la wapiganaji wa Boko Haram.
null
Gavan wa jimbo la Kaduna amewaonya wenyeji kuwa waangalifu sana na kuepuka maeneo yaliyojaa watu kwani hayo ndio yanayolengwa na washambuliaji wa kujitolea mhanga.
null
Gavana Nasir El-Rufa'I amewasihi wenyeji waepuke misikiti makanisa masoko na vituo vya mabasi hadi pale hali itakapotulia.

Inspekta wa polisi wa Nigeria ameomba wanigeria kuwa makini na waangalifu akisema kuwa ''kwa sasa inaonekana mabomu yameundwa mengi na kwa hakika likishaundwa bomu ni vigumu sana kuzuia mashambulizi ya kujilipua kwenye umati wa watu ilikuzidisha maafa''.


Tayari hofu imetanda katika mji wa Abuja ambapo Polisi wamepiga marufuku uuzaji na uchuuzi katika barabara za katikati ya mji.
kutoka BBC
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment