Washambuliaji wawili wa kujitoa mhanga
waliojilipua katika uwanja wa ndege wa Brussels Jumanne wametambuliwa kuwa
ndugu wawili, Khalid na Brahim el-Bakraoui.
Kituo cha runinga cha RTBF kimesema wawili hao walifahamika
vyema na polisi.
Mwanamume wa tatu aliyeonekana kwenye video za kamera za
siri uwanja wa ndege akiwa pamoja na wawili hao bado anasakwa.
Milipuko miwili ilitokea katika uwanja wa ndege na mwingine
mmoja katika kituo cha treni na kuua watu 34 na kujeruhi wengine 250.
§ Kwa Picha: Mashambulio ya Brussels
Ubelgiji imeanza siku tatu za maombolezo ya kitaifa.
RTBF imesema ndugu hao wawili walifahamika na polisi na wana
rekodi za uhalifu lakini hawakudhaniwa kuwa na uhusiano na ugaidi awali.
Kituo hicho cha runinga
kimesema Khalid el-Bakraoui alitumia jina bandia kukodi nyumba katika eneo la
Forest jijini Brussels ambapo polisi walimuua mtu mwenye silaha kwenye
makabiliano wiki iliyopita.
Ilikuwa ni wakati wa msako huo ambapo
polisi walipata alama za vidole za Salah Abdeslam, mshukiwa mkuu wa mashambulio
ya Paris ya 13 Novemba.
Abdesalam alikamatwa kwenye operesheni
ya maafisa wa usalama Ijumaa.
Kutoka BBC Swahili
0 maoni:
Post a Comment