MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

WASHUKIWA SITA WAKAMATWA BRUSSELS

Brussels
Polisi nchini Ubelgiji wamewakamata washukiwa sita mjini Brussels huku uchunguzi ukiendelea kuhusu mashambulio ya Jumanne yaliyosababisha vifo vya watu 31.
Watu hao walikamatwa katika mtaa wa Schaerbeek.
Polisi bado hawajatoa majina yao na pia hawajasema iwapo walihusika katika mashambulio hayo.
Kwingineko Ufaransa, mshukiwa ambaye inasadikika alikuwa akipanga shambulio amekamatwa karibu na mji wa Paris, maafisa wamesema.
Mashambulio hayo ya Brussels yamehusishwa na mashambulio ya Paris ya Novemba mwaka jana.
Kundi linalojiita Islamic State (IS) limekiri kutekeleza mashambulio yote mawili.

 


 KUTOKA BBC Swahili
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment