Wapiganaji wa kundi la Boko Haram
wameishambulia kambi ya jeshi la Nigeria mapema asubuhi ya leo na kuua idadi
kubwa ya wanajeshi huko Borno.
Mwanajeshi mmoja aliyeko
Borno ameielezea BBC kuwa''wapiganaji wa Boko Haram waliwavizia na
kuwashambulia alfajiri na mapema wakiwa wamelala.''
''Wapiganaji hao walikuwa wamejihami kwa
silaha kali na kusababisha maafa makubwa upande wa wanajeshi''
Kambi hiyo ndogo iliyoko
katika kijiji cha Kareto ilikuwa na wanajeshi wachache ambao kazi yao ilikuwa
ni kulinda ngome kabla ya kikosi kikubwa zaidi kuwasili.
Hata hivyo mwanajeshi huyo anasema kuwa
idadi ya wapiganaji hao ilikuwa kubwa mno hata wanajeshi kadhaa walitoroka
ilikuokoa maisha yao.
''Walikuwa na silaha nzito nzito na kali
kuliko zetu'' afisa huyo aliiambia idhaa ya BBC Hausa.
''Tuliwapoteza wenzetu
wengi,,,,,wengi sana,, sijui hata ni wangapi waliojeruhiwa''
''Baadhi yetu walitoroka maji yalipozidi
unga''
''Tuligundua idadi ya wavamizi ilikuwa
ni kubwa kuliko yetu'' mwanajeshi mwengine aliiambia shirika la habari la AFP.
Wapiganaji kadhaa
waliuawa katika makabiliano hayo yaliyodumu kwa saa kadhaa kulingana na wenyeji
wa kijiji hicho.
Hata hivyo jeshi lilijitahidi na
kuikomboa kambi hiyo baada ya mashambulizi ya angani kuwasili na kuwaokoa
wanajeshi walikuwa wamesakamwa ardhini.
Idadi kamili ya waliouawa haijajulikana.
kutoka <a>BBC Swahili.com
0 maoni:
Post a Comment