Mgombea wa urais nchini
Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican Donald Trump ameahidi kubadilisha
sifa zake katika mkutano wa faragha na viongozi wa Republican.
Mfanyibishara huyo
ambaye yuko kifua mbele katika kuwania urais kupitia chama hicho alitoa ujumbe
wake kupitia wasaidizi wake ,kulingana na chombo cha habari cha AP.
Kuimarika kwake katika
mchujo huo kufikia sasa kumetuma ishara miongoni mwa viongozi wa chama hicho
kwamba matamshi pamoja na sera zake huenda zisiwavutie wapiga kura.
Majimbo matano yanapiga
kura siku ya Jumanne kumchagua mgombea wao wa urais.
Bwana Trump ana uongozi
mkubwa wa idadi ya wajumbe lakini huenda asipate wajumbe 1,237 anaohitaji
kushinda mchujo huo bila ya mkutano wa wanachama.
Wasaidizi wamewaambia
viongozi wa chama kwamba amekuwa akibadilisha sifa zake na kwamba hatua hiyo
imeanza kufua dafu.
kutoka BBC Swahili
0 maoni:
Post a Comment