MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

DONALD TRUMP, KUBADILI SIFA ZAKE

Mgombea wa urais nchini Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican Donald Trump ameahidi kubadilisha sifa zake katika mkutano wa faragha na viongozi wa Republican.

Mfanyibishara huyo ambaye yuko kifua mbele katika kuwania urais kupitia chama hicho alitoa ujumbe wake kupitia wasaidizi wake ,kulingana na chombo cha habari cha AP.

Kuimarika kwake katika mchujo huo kufikia sasa kumetuma ishara miongoni mwa viongozi wa chama hicho kwamba matamshi pamoja na sera zake huenda zisiwavutie wapiga kura.

Majimbo matano yanapiga kura siku ya Jumanne kumchagua mgombea wao wa urais.

Bwana Trump ana uongozi mkubwa wa idadi ya wajumbe lakini huenda asipate wajumbe 1,237 anaohitaji kushinda mchujo huo bila ya mkutano wa wanachama.


Wasaidizi wamewaambia viongozi wa chama kwamba amekuwa akibadilisha sifa zake na kwamba hatua hiyo imeanza kufua dafu.

kutoka BBC Swahili
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment