Badala yake hutumia muda huo kujihudumia
kwenye gesti, baa, kulala na katika shughuli za starehe.
Serikali imesema hali hii inaichelewesha
Tanzania kuingia katika kundi la mataifa yenye uchumi wa kati kufikia mwaka
2025.
Bi Ruth Minja, ambaye ni mtakwimu mkuu
katika ofisi ya taifa ya takwimu Tanzania, ndiye aliyeongoza utafiti huo wa
watu wenye uwezo wa kufanya kazi kwa mwaka 2014/2015.
Anasema waligundua kuwa watu wenye uwezo wa kufanya kazi
walikuwa milioni 25 kutokana na kiashiria cha saa za kufanya kazi kupungua na
baadhi ya wafanyakazi kupunguzwa kazi kutokana na utendaji dhaifu.
Ally Msaki, aliyemuwakilisha katibu mkuu katika ofisi ya waziri
mkuu anayeshughulikia masuala ya kazi,vijana ajira na watu wenye ulemavu
amewaangazia Watanzania walioko kwenye ajira, ambao wanapata kipato ambacho
hakitoshelezi kuweza kumudu gharama za maisha.
Amesema nafasi kama hizo za kazi hazina viwango vya ubora na ni
kinyume cha maelekezo ya shirika la wafanya kazi duniani ILO.
Ingawa Sera ya taifa ya ajira kwa Taifa la Tanzania kwa mwaka
2008 ilijikita zaidi katika kuongeza fursa za ajira na kufanikiwa katika lengo
lake, kuna kasoro kwenye kipengele cha ubora wa ajira.
chanzo BBC Swahil.
0 maoni:
Post a Comment