MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

D’Banj: Ndoa yangu haiwahusu, niacheni!

Wiki kadhaa zilizopita, D’Banj alitengeneza vichwa vya habari baada ya kudaiwa kuwa amefunga ndoa kisiri na mpenzi wake, Lineo Didi Kilgrow.
Dbanj-new

Tangu hapo, muimbaji huyo amekuwa kimya kuhusiana na suala hilo hadi Jumamosi iliyopita alipozungumza na Saturday Beats.

Akizungumza kuhusu ndoa yake, muimbaji huyo alisema maisha yake binafsi hayahusianI na mtu yeyote na kuwaomba watu kuyaacha maisha ya familia yake faragha.

“Ndoa yangu ni mambo yangu na si mambo ya mtu mwingine. Kama nimeoa ama sijaoa, fuatilia mambo yako. Kama ukija kuona pete ya ndoa kwenye kidole changU, sawa, lakini kama huoni, sawa,” alisema.
“Ukweli kuhusu hilo ni kwamba ni muhimu sana kujua unachotaka kama brand. Kama brand, nilitaka kujikita kwenye upande wa biashara na kuweka familia na maisha binafsi faragha,” aliongeza msanii huyo.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment