MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

Marekani kufanya majaribio ya kudungua kombora

 Mfumo wa kudungua makombora wa Marekani uliopelekwa Korea Kusini
Idara ya jeshi nchini Marekani kwa mara ya kwanza itajaribu kudungua kombora la masafa marefu lililo na uwezo wa kufyatuliwa kutoka bara moja hadi bara lingine.

Maafisa wa Pentagon wanasema jaribio hilo litafanyika Jumatano, wiki ijayo.

Kumekuwa na wasiwasi mjini Washington kuhusu uboreshaji wa miradi ya kinyuklia na makombora ya masafa marefu ya Korea Kaskazini.

Mkuu wa shirika la ujasusi la Marekani anasema iwapo miradi ya Korea Kaskazini ya kutengeneza makombora haitodhibitiwa, basi taifa hilo lina uwezo wa kutengeneza kombora lenye uwezo wa kufikia Marekani.

Kutoka BBC Swahili.com
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment