MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

AMISOM ITAUHAMA UWANJA WA MOGADISHU

        
Kikosi cha amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia, AMISOM, kimekubali ombi la
 Shirika la Kandanda la Somalia kuhama kutoka uwanja wa mpira wa Mogadishu,
 ili uwanja huo upate kufanyiwa ukarabati kuweza kutumiwa tena kama pahala pa michezo.
Mogadishu stadium

Msemaji wa AMISOM, Kanali Ali Adan Hamud, alisema AMISOM imekaribisha ombi hilo na
 kwamba AMISOM imeamua kuondoka kwenye uwanja huo ufikapo mwezi wa Disemba
mwaka huu.

Uwanja huo umekuwa kambi ya askari wa AMISOM tangu Agosti mwaka jana.

Kabla ya hapo ukitumiwa na wapiganaji wa Al-Shabab na mapambano makali yamewahi
kutokea kwenye eneo la uwanja huo.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment