UHARAMIA WAPUNGUA PWANI YA SOMALIA
Idadi ya meli zinazotekwa na maharamia katika pwani ya Somalia, zimepungua sana mwaka huu , kulingana na shirika la kimataifa la safari za majini.
Ni meli sabini pekee zilitekwa nyara katika miezi ya kwanza tisa mwaka huu ikilinganishwa na visa 233 vilivyoripotiwa mwaka 2011.
Juhuzi za kimataifa pamoja na mikakati kipya ya kiusalama ndiyo imekuwa changamoto kubwa kwa maharamia kuendesha kazi zao kulingana na shirika hilo.
Lakini shirika hilo limetoa tahadhari kwa mabaharia kuwa makini wakati wa shughuli zao hasa katika pwani ya Somalia
Mkurugenzi wa shirika hilo, Kapteni Pottengal Mukundan, alisema ni habari njema kusikia kuwa uharamia umepungua, lakini mabaharia hawapaswi kulegea katika kuchukua tahadhari.


0 maoni:
Post a Comment