MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

KIKOSI CHA ZANZIBAR CHAFUNGIWA
Shirikisho la mchezo wa Soka visiwani Zanzibar,ZFA limechukua uamuzi ambao umewashngaza sana mashabiki wengi wa soka, visiwani humo, nchini Tanzania na barani Afrika kwa ujumla.
Kwa mujibu wa ripoti maafisa wakuu wa ZFA wamewapiga marufuku wachezaji wake wote walioshiriki katika michuano ya kuwania kombe CECAFA Senior Challenge, iliyokamilika nchini Uganda, kutoshiriki katika mechi yoyote popote duniani kwa muda usiojulikana.
Aidha ZFA limeamua kuvunja timu ya taifa maarufu kama Zanzibar Heroes, licha ya kuwa timu hiyo ilimaliza katika nafasi ya tatu katika michuano hiyo ya CECAFA.
Baadhi ya wachezaji hao waliopigwa marufuku ni pamoja na nyota na naodha wa Yanga, Nadir Haroub.

Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment