MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG


SHIRIKISHO la Soka Barani Africa (CAF), linatarajia kutuma mjumbe wake kwa ajili ya kuja kukagua klabu zote zinazoshiriki michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara, kwa ajili ya kupewa leseni za kushiriki michuano ya CAF.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaa jana, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Bonifasi Wambura, alisema mjumbe huyo kutoka CAF atafika nchini Januari 7 kwa ajili ya kufanya ukaguzi huo.

“Ili klabu iweze kupewa leseni ya CAF kwanza klabu inatakiwa iwe na viongozi walioajiriwa, iwe na uwanja wake wa mazoezi pamoja na anuani pamoja na ofisi ya klabu pamoja na programu za vijana ,” alisema Wambura.

Wambura pia alisema kwa klabu za Simba na Azam ambazo zinashiriki katika michuano ya Klabu bingwa Afrika na Kombe la Shirikisho zenyewe zinatakiwa kuonyesha hotel zitakazotumiwa na wageni wao wakati wa michuano hiyo.

Mjumbe huyo kutoka CAF anatarajiwa kuanza kazi hiyo Januari 7 hadi 14 mwakani.

Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment