MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

MR NICE, TENA KWENYE MGOGORO NA LEBO YAKE MPYA

Mr Nice, ameingia tena katika mgogoro na lebo yake ya sasa huko nchini Kenya, inafuatiwa na kile kinachosadikika kuwa msanii huyo na lebo hiyo kuna baadhi ya mambo hawakuwa wanakubaliana katika kushauriana.
Mkurugenzi wa lebo ya Candy and candy Records, alisema kuwa walitofautiana mara baada ya kampuni kutaka kazi zenye ubora kutoka kwa msanii huyo, aliendelea kwa kusema kuwa Mr Nice, ni msanii anayependwa sana hasa Mombasa, lakini siku chache zilizopita tulikuwa katika mabishano kidogo hii ilitokana na mtazamo tofauti hasa ni kutokana na wimbo wake mpya wa Akina Mama, binafsi ule wimbo sikuupenda na nilimshauri kwamba ni vyema tungetumia wimbo mwingine, lakini aligoma.
Wimbo huo haukupendwa kabisa na wadau na mashabiki wa muziki nchini humo, hayo yalikuwa maneno ya meneja wa Mr Nice.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment