MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

RPMA MKATOLIKI, AMEFUNGUKA KUHUSU “KKK” NA THE RETURN OF THE NINJA PROJECT.

Audio: Roma kutoa wimbo mpya wiki ijayo
Msanii wa hip hop , Tanzania, kutoka Tongwe Records, Roma Mkatoliki, amefunguka na kusema kuwa yuko mbioni kuachia ngoma yake mpya wiki ijayo, jina la ngoma hiyo ni “KKK” ikiwa ni katika Project yake mpya ya “ The Return of The Ninja”...........


“Tunaplan kuitoa siku yoyote kuanzia wiki ijayo yaani kuanzia jumatatu. Inaweza kuwa Jumatatu hiyo hiyo ama jumanne, ama jumatano. Kwa nini hatuko sure…kwa sababu Tongwe kuna wasanii wengi ambao wanatakiwa kutoka pia...ndo maana hatuko sure na tarehe lakini tuko sure na wiki. Wimbo utatoka wiki ijayo, unaitwa ‘KKK’ yaani triple K, umefanyika Tongwe records kwa producer J-Ryder pamoja usimamizi mzima wa C.E.O wetu wa Tongwe ambaye ni J-Marder.” Alifunguka  Roma.

Aliendelea kwa ufafanuzi zaidi “Kilichofanyika ni kwamba 2030 ndo ni kama nilikuwa nimefunga hivi kitu ambacho nilikuwa nimekianza, nikiwa ninamaanisha kwamba kama ni album ambayo ilikuwa inatakiwa kutoka basi ilifungwa kwa kutoa 2030 ambayo niliitoa mwaka 2012 mwishoni kuelekea 2013.” Roma aliiambia The Jump Off.
“Kwa takribani miaka sita ama saba nilikuwa na system hiyo ya kutoa wimbo mmoja kwa mwaka toka 2007 tunaanza na wimbo wa kwanza. Lakini time inaenda na vitu vingi vinaenda vinabadilika. Kwa hiyo kitu ambacho Roma anakuja nacho 2014 hatatoa wimbo mmoja kama ilivyozoeleka, nina plan ya kutoa nyimbo kama tatu kwa sababu nyimbo zinarekodiwa kila siku. Kwa hiyo wimbo wa kwanza tunautoa mwanzo wa mwaka, katikati ya mwaka kwenye June hivi naweza kutoa wimbo mwingine na mwishoni mwa mwaka naweza kutoa wimbo mwingine.” Hayo yalikuwa maneno ya  Roma.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment