MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

NIGERIA:HATUHITAJI MSAADA WA UN

Nigeria haihitaji msaada wa Vikosi vya Umoja wa Mataifa kupambana na Boko Haram.Mshauri wa maswala ya usalama wa taifa nchini humo ameiambia BBC................


Sambo Dasuki amesema Nigeria na majirani zake Niger,Chad na Cameroon wanamudu kusshughulikia swala la Wanamgambo wa kiislamu.

Dasuki amekiri kuwa Wanamgambo ni tishio kubwa la usalama nchini humo na kusema kuwa takriban asilimia 50 ya Jeshi la Nigeria limepelekwa kaskazini mashariki .

Amesema hatua hiyo inaashiria namna Jeshi lilivyolichukulia swala hili kwa umakini mkubwa.

Alipoulizwa na Kipindi cha Newsday cha BBC kama Nigeria inahitaji msaada wowote wa nje , alisema ''hapana''

Wanamgambo wa Boko Haram walianza Operesheni yao mwaka 2009, wakidai kuwa wanataka kuunda taifa la kiislamu.


Tangu Serikali ilipotangaza hali ya hatari miezi 20 iliyopita kaskazini mashariki ili kupambana na Wanamgambo, kundi hilo limejiimarisha na sasa linadhibiti miji kadhaa .
kutoka BBC
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment