MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

Ndege za kivita za Marekani zapaa Korea

 Ndege za jeshi la Marekani aina ya B-1B zikipaa juu ya Pyeongtaek, Korea Kusini 13 Septemba, 2016.
Ndege mbili za kivita za Marekani zenye uwezo wa kubeba silaha za nyuklia, B-1 Lancer, zimepaa juu ya anga ya Korea Kusini, siku chache baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la tano la silaha za nyuklia.

Ndege hizo zilipaa si mbali sana kutoka ardhini juu ya kituo cha kijeshi kinachopatikana kilomita 77 kutoka mpaka wa Korea Kaskazini na Korea Kusini.

Marekani imeitahadharisha Korea Kaskazini kwamba hatua kali zitachukuliwa dhidi ya taifa hilo baada ya kufanyika kwa majaribio hayo ya bomu Ijumaa.

Kutoka BBC Swahili
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment