MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

Monaco wamchukua Jovetic kutoka Inter

Stevan JoveticHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionStevan Jovetic alikaa nusu ya msimu uliopita Sevilla
Mabingwa wa ligi kuu ya Ufaransa Ligue 1 Monaco wamemnunua mshambuliaji anayetoka Montenegro Stevan Jovetic kutoka klabu ya Inter Milan ya Italia kwa dau la £10m.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu ya Manchester City ametia saini mkataba wa miaka minne.
Jumatatu, picha za Jovetic, 27, akiwa amevalia jezi nambari 10 ambayo awali ilivaliwa na Kylian Mbappe zilianza kutokea mtandaoni.
Mbappe anadaiwa kukaribia kujiunga na Paris St-Germain kwa mkono.
"Nina furaha sana kuwa hapa. Kuna wachezaji wazuri sana katika timu hii. Ndio maana nikaichagua AS Monaco,2 aliambia tovuti ya Monaco.
Inaarifiwa kuwa Mbappe, 18, atajiunga na PSG kwa mkopo kabla ya dirisha la kuhama wachezaji kufungwa Alhamisi na baadaye atakamilisha uhamisho wa kudumu majira yajayo ya joto kwa euro 180m (£167m).
Mpango huo utaiwezesha kampuni hiyo ya Paris kutimiza matakwa ya sheria ya uchezaji haki kifedha baada yao kuvunja rekodi ya dunia kumnunua Neymar
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment