MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

Mzozo wa Korea Kaskazini na Marekani kwa muktasari

Image from North Korean media of four missile launches on 7 March 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Mzozo unaohusisha Korea Kaskazini ni mzozo ambao unaweza hata kusababisha vita vya vinyuklia, vita ambavyo huenda pengine haviwezi vikawa na mshindi. Lakini ni mzozo wenye mambo mengi tata. Hebu tuchanganue kiasi.

Ni kwa nini Korea Kaskazini inataka silaha za nyuklia?

Rais ya Korea iligawanyika na kuwa mataifa mawili baada ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia na kukawa na Korea Kaskazini na Kusini. Korea Kaskazini iliegemea siasa za Kikomunisti na iliongozwa na serikali ya kiimla, uongozi sawa na wa Stalin katika Muungano wa Usovieti. Marafiki wake wakuu ni Urusi na Uchina.
Nchi hiyo ilijitenga pakubwa na nchi nyingine, isipokuwa nchi kadha marafiki wake. Viongozi wa nchi hiyo wanasema silaha za nyuklia ndiyo njia pekee ya kujikinga dhidi ya maadui kutoka nje ambao wanataka kuliangamiza taifa hilo.

KUTOKA BBC
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment