MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG


KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), leo imefanya  mkutano wake utakaokuwa na ajenda mbili katika kikao hiko.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Afisa Habari wa TFF Bonifasi Wambura, alisema kutakuwa na ajenda mbili katika kikao hiko ambalo moja ni kuhusu mkutano mkuu wa uchaguzi wa TFF.

“katika kikao hiko cha kesho (leo), ajenda kuu ni kuhusu swala la mabadiliko ya katiba mpya ya TFF, ambapo kamati itapitia walaka zilizotolewa kwa vyama wanachama wa TFF kwa ajili ya kupiga kura mchakato huo.

Na pia ajenda nyingine katika kikao hiko itakuwa ikihusiana na mkutano wa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa TFF,” alisema Wambura.

Wakati huo huo Wambura, aliupongeza uongozi mpya wa Chama cha Soka Mkopa wa Dar es Salaam (DRFA), baada ya kushinda katika uchgaguzi wake mkuu uliofanyika Juma tano.

“Tunaimani kabisa uongozi uliochaguliwa na wajumbe wa DRFA, watatenda kazi kwa mujibu wa katiba ya chama hiko,” alisema
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment