Anas Al-Liby aliyekamatwa na wanajeshi wa Marekani mjini Tripoli kwa
kuhusika na mashambulizi ya kigaidi dhidi ya balozi za Marekani mwaka 1998
amekausha madai ya ugaidi dhidi yake.
Abu Anas al-Liby, ambaye jina lake halisi ni Nazih Abdul-Hamed
al-Ruqai, alikanusha madai dhidi yake kupitia kwa wakili wake.
Anatuhumiwa kwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la al-Qaeda
na kupanga mashambulizi ya kigaidi dhidi ya balozi za Marekani nchini Kenya na
Tanzania mwaka 1998.
Watu zaidi ya 220 walipoteza maisha yao.
Bwana Liby, mwenye umri wa miaka 49, alisemekana kuwa na kesi ya
kujibu mwaka 2000.
Siku ya Jumanne Liby alionekana akiwa amefungwa pingu mkononi
katika mahakama moja mjini New York.
Liby, alisikiza kwa maakini jaji akimusomea mashitaka dhidi yake
.
Baadaye alikanusha madai hayo dhidi yake na jaji akaakhirisha
kesi hiyo hadi Oktoba 22.
Mshukiwa aliondoshwa mahakamani baada ya jaji kusema muwa lazima
aendelee kuzuiliwa kwani kuna tisho la yeye kutoroka.
Kumekuwa na ghadhabu nchini Libya tangu makomando wa Marekani
kumkamata al Liby anayedaiwa kuwa mmoja wa viongozi wa kundi la Al Qaeda mjini
Tripoli mapema mwezi Oktoba.
Wengi walikiona kitendo hicho kama cha kutoheshimu uhuru wa
Libya.
Hata hivyo Marekani kupitia kwa waziri wake wa mambo ya nje John
Kerry imesema kuwa Liby alikuwa mshukiwa halali aliyepaswa kukamatwa.
Hata hivyo serikali ya Libya baada ya kukamatwa kwa Liby
ilimtaka balozi wa Marekani nchini humo kueleza kwa nini ilifanya hivyo
Waziri mkuu wa Libya Al Zeydan ambaye alitekwa nyara kwa masaa
kadhaa siku chache baada ya Al Libya kukamatwa, alisema kuwa wahalifu wenye
uraia wa Libya wanapaswa tu kushitakiwa na kuhukumiwa ndani ya nchi hiyo
Majasusi walimuhoji Libya kwenye mali ya kijeshi kwa wiki moja
kabla ya kumpeleka mahakamani huku wanawe wakisema kuwa serikali ilihusika
katika kukamatwa kwake, madai ambayo serikali imekanusha.
Kutoka BBC
0 maoni:
Post a Comment