Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya
Newcastle United Faustiano Asprilla, amepewa ofa ya kuigiza Filamu ya za Ngono
na kampuni moja inayojihusisha na utengenezaji wa filamu hizo nchini Colombia.
Asprilla
amepewa ofa ya Peso Milioni 20 sawa na dola 10,000. Ambazo atalipwa mara baada
ya kusaini mkataba wa wiki moja tu.
Kampuni
ya Santa Latina ambayo ni moja ya kampuni zinazoongoza kwa utengenezaji wa
Filamu za Ngono nchini Colombia, imevutiwa na muonekano wa mshambuliaji huyo
mwenye umri wa miaka 43, na kutaka kumpa shavu la wiki moja tu.
Mpaka
sasa mchazaji huyo bado hajasema chochote au kujibu maombi hayo.
0 maoni:
Post a Comment