Wakenya wameghadhabishwa sana na hatua ya wanaume watatu waliombaka
msichana mmoja na kutupa mwili wake kwenye choo kuamrishwa na polisi kukata
nyasi kama adhabu kwao.
Msichana huyo alishambuliwa na kubakwa akiwa njiani kutoka kwa
mazishi ya babu yake katika kijiji kimoja Magharibi mwa nchi.
Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la Daily Nation nchini Kenya,
uti wa mgongo wa msichana huyo ulivunjika wakati wa ubakaji na sasa amelazimika
kutumia kiti cha magurudumu.
Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu pamoja na wabunge
wamelaani polisi kwa kukosa kuchunguza madai ya msichana huyo.
0 maoni:
Post a Comment