Mandela atazikwa tarehe 15 mwezi Disemba |
Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma ametangaza mazishi ya
Nelson Mandela yatafanyika siku ya Jumapili, Desemba 15 mwaka huu kijijini
kwake Qunu, katika jimbo la Eastern Cape, Afrika Kusini.
Rais Zuma ametangaza siku 5 za maombolezo kitaifa na
bendera zitapeperushwa nusu mlingoti katika muda wote huo. Na ameitangaza siku
ya Jumapili ya Desemba 8, 2013 kuwa siku maalumu ya kitaifa ya maombolezo na
kumkumbuka Madiba nchi nzima.
Tayari msisimko wa mazishi hayo yanayotarajiwa kuwa ya
kihistoria umekamata dunia nzima, ambapo tayari Rais Obama wa Marekani, mstaafu
Bill Clinton na Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron ni baadhi tu ya viongozi
ambao wamethibitisha kushiriki.
Sala ya mazishi imepangwa kufanyika katika Uwanja wa
Taifa wa FNB Desemba 10, 2013 jijini Johanesburg.
Mwili wake utawekwa katika jengo la serikali liitwalo
Union Buildings kuanzia Desemba 11 hadi 13, kwa kupewa heshima za mwisho, kabla
ya kupelekwa kijijini Qunu kwa mazish
0 maoni:
Post a Comment