MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

S.KUSINI : 200 WAZAMA MTO NILE


 
 Zaidi ya watu 200 raia wa Sudan Kusini wamezama katika ajali ya boti kwenye mto Nile wakikimbia vita vinavyoendelea katika mji wa Malakal.

Taarifa hii ni kwa mujibu wa msemaji wa jeshi la Sudan Kusini.
Boti hiyo iliyozama, ilikuwa imewabeba watu wengi kupindukia. Watu hao walikuwa wanatoroka vita vinavyotokota katika mji wa Malakal.

Mapigano yalizuka Sudan Kusini mwezi Disemba mwaka jana baada ya Rais Salva Kiir kumtuhumu aliyekuwa makamu wake wa Rais Riek Machar, kwa kuwa na njama ya kumpindua.

Umoja wa Mataifa unasema kuwa zaidi ya watu 1,000 wameuawa tangu ghasia kuanza nchini humo.
Kutoka BBC
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment