Mashirika ya
kutoa misaada yameonya kuwa endapo raia wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati ambao ni Waislamu, wataendelea
kuihama taifa hilo, masoko ya nchi hiyo huenda yakasambaratika kabisa.
Mashirika ya kutoa misaada ya Oxam na lile la Action against hunger yamesema kuwa chini ya maduka kumi ya jumla ndiyo yalisosalia katika mji mkuu wa nchi hiyo na kuwa wafanyabiashara wengi wanaendelea kutoroka taifa hilo.
Kufuatia hali hiyo mashirika hayo yameonya kuwa hazina ya vyakula huenda ikapungua kwa kiasi kikubwa na kuwa bei ya vyakula huenda ikapanda zaidi.
Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa zaidi ya asilimia tisini ya rais wa nchi hiyo, wanaishi kwa kula chakula mara moja kwa siku na kuwa hali hiyo huenda ikawa mbaya zaidi.
Taifa hilo
limegawanyika zaidi kufuatia vita vilivyoanza mwaka uliopita kati ya Wakristu
ambao ni wengi nchini humo na Waislamu kufuatia mapinduzi ya serikali.
Maelfu ya Waislamu tayari wametoroka nchini humo na
kutafuta hifadhi katika mataifa jirani ya Cameroon
na Chad.
Upungufu wa chakula
Kwa sasa kuna upungufu mkubwa wa nyama kwa sababu
wafugaji wamekimbilia msituni na wakati wanapochinja mifugo wao, bei yake ni
ghali mno.
Wengi wa Waislamu waliofukuzwa na Wakristu walikuwa
wakichangia pakubwa katika uchumu wa taifa hilo.
Ghasia zinazoendelea zimezuia vyakula kuingizwa nchini humo na ripoti zinasema kuwa mamia ya malori yaliyosheheni chakula yamekwama katika mpaka wa nchi hiyo na Cameroon, kwa sababu madereva wengi wana wasi wasi wa kushambuliwa na makundi yaliyojihami.
Shirika hilo la Oxfam, limesema kuwa endapo raia waliosalia hawatapewa ulinzi wa kutosha, hali nchini Jamuhuri ya Afrika ya Kati huenda ikawa mbaya zaidi.
kutoka BBC Swahili to www.mweraamazing.blogspot.com
0 maoni:
Post a Comment