Mwimbaji wa kike wa bongo flava mwenye mafanikio makubwa, Judith
Wambura aka Lady Jay Dee amebreak habari njema kwa mashabiki wake wa mitandao
ya kijamii ambao wanafikia 225,722 kwa upande wa Facebook na zaidi ya 66, 400
wanaomfuata kwenye Twitter, kuwa ataitoa rasmi video ya wimbo wake wa
‘Historia’, February 8 mwaka huu kupitia party maalum, na watu 20 kati yao
watapata nafasi ya kuhudhuria tukio hilo.........
“Video ya Historia iko
tayari na itatoka Jumamosi ya tar 8 february 2014 kwenye party maalum ya
kuitambulisha, na kutoka humu facebook nitaalika watu 20 wa kuja kuiangalia kwa
mara ya
kwanza kabla haijaruka kwenye TV zote.. Swali litakuja na 20 wa mwanzo
watakaopatia nitajumuika nao. Usicheze mbali.” Ameandika Lady Jay Dee.
0 maoni:
Post a Comment