Mahakama nchini Ufaransa, imemhukumu kifungo cha miaka 25 jela jasusi
mkuu za zamani wa Rwanda
Pascal Simbikangwa kwa
kuhusika na mauaji ya kimbari mwaka 1994........
Simbikangwa alipatikana na hatia ya kuhusika na mauaji hayo na kutenda uhalifu dhidi ya binadamu.
Alikabiliwa na makosa ya kuchochea , kupanga na kusaidia katika juhudi za mauaji ya watutsi hasa kwa kuwapa silaha wapiganaji wa kihutu waliokuwa wanalinda vizuizi vya barabarani na kuwaua wanaume wa kabila la Tutsi, wanawake na watoto.
Simbikangwa alikanusha madai hayo.
Haijuikani kama mawakili wa Simbikangwa watakata rufaa dhidi ya uamuzi huo.
0 maoni:
Post a Comment