Kampuni ya Apple, imeamua kuwasaidia watumiaji wa
bidhaa zake za simu kwa kuweka program itakayomuwezesha mtumiaji wa simu kutuma
au kusoma ujumbe huku akiwa anatembea na wala hautoweza kujikwaa au kugongana
na mtu. Pia unaweza kuendesha gari ukiwa unatuma au kusoma ujumbe katika simu
yako..........
Kampuni hiyo itaongeza “patent” kwenye simu zake
itakayokuwa inaonesha Live Video kwenye background ya uwanja wa kuandikia
ujumbe, Kifaa hicho kitatumia kamera ya simu, ambayo itakuwezesha kuona vitu
vyote vya mbele yako kupitia kio cha simu yako ya mkononi wakati ukiwa
unaandika ujumbe wako.
0 maoni:
Post a Comment