Ice Cube, amefunguka na kuziponda Tuzo za MTV, kwa kumpa
marehemu Paul Walker, na Vin Diesel, tuzo za “Best Onscreen Duo” ............
Ice Cube ameliambia gazeti la USA Today kuwa Paul Walker alipewa tuzo hiyo kwa
sababu tu ya huruma na sio vinginevyo lakini tuzo hiyo alistahili kupewa yeye
na Kevin Hart kupitia comedy yao
ya ‘Ride Along’.
Aliendelea kwa kusema kuwa “Aibu yenu, MTV.” Alisema
Ice Cube. “Tulikuwa na chemistry bora zaidi kuliko wote waliokuwa nominated,
sisi kutoshinda ilikuwa ajabu. Tulikuwa ‘The Best Onscreen Duo’.
Pia aliweka sawa kauli yake kwa kusema kuwa “Walipaswa
kumpa kabla hajafariki” .
Rapper huyo alieleza kutofurahishwa kabisa na jinsi
ambavyo tukio la utoaji tuzo lilivyoendeshwa kiasi cha kuondoka kabla ya show
kuisha.
“Sikuwa nafurahishwa. Nimekuwa nikiingia ndani na nje
ya vitu kama hivi kwa miaka 25. Kama
haufurahishwi, kwa nini ujitese. Punde unapoona zinakuboa, amka na ondoka.”
0 maoni:
Post a Comment