MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

KOCHA WA KIKOSI CHA TIMU YA TAIFA YA ITALIA, AMEJIUZULU KUFUNDISHA TIMU HIYO, SABABU ZIKO HAPA



 20140625-080553-29153617.jpg
Kichapo walichopatiwa kikosi cha Italy,kilichopelekea timu hiyo kuyaaga michuano ya kombe la Dunia Huko nchini Brazil, kumepeleke Timu hiyo kumpoteza kocha wake. Cesar Prandelli..............

                                       
Timu ya Italy, imetolewa nje ya michuano hiyo baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0, katika mchezo uliochezwa hapo jana kati ya Italia na Uruguay, baada ya kichapo hicho Kocha wa Timu hiyo alikuwa na mkutano na waandishi wa habari, alitangaza kujiuzulu kuifundisha timu hiyo.

“Nilichagua mfumo fulani wa ukufunzi na ndio sababu ninajiuzulu, kwa sababu haukufanya kazi,” alisema.

Aliendelea kwa kusema kuwa: “Kuna jambo ambalo limebadilika tangu nilipotia saini mkataba mpya. Sijui kwanini lakini sina haja ya kutafuta sababu .”

Prandeli amechukua hatua hii baada ya kujiuzulu kwaa rais wa shirikisho la kandanda la Italia Giancarlo Abete.
“Nilizungumza na rais wa shirikisho na naibu wa rais Demetrio Albertini na nikawapa barua ya kujiuzulu kwangu. Ni jambo lisilobadilika,”

Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment