Kimbunga kikali kimekumba kisiwa cha
Vanuatu katika kile umoja wa mataifa unasema kinaweza kuwa janga baya zaidi
kuwahi kulikumba eneo la pacific.
Kuna
hofu kuwa huenda idadi ya watu waliokufa ikaongezeka.................
Kimbunga
hicho kwa jina Pam kilikuwa na upepe unaovuma kwa kasi ya kilomita 250 kwa saa
, mvua nyingi na upepo mkali.
Kimeng'oa
paa za nyumba na miti na kukata nguvu za umeme.
Mawasiliano
yametatizika na huenda uharibifu sehemu zingine utajulikana baada ya siku
kadhaa.
Maelfu
ya watu walikimbilia usalama kwenye kambi za muda lakini wengine walisalia
makwao
Kimbunga
hicho tayari kimesababisha uharibifu mkubwa maeneo mengine ya kusini mwa
pacific vikiwemo visiwa vya kiribati na Solomon.
Kutoka BBC.
0 maoni:
Post a Comment