Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa
Francis amedokeza kwamba huenda akafuata nyayo za mtangulizi wake Papa Benedict
kwa kujiuzulu.............
Akihojiwa
na runinga moja ya nchini Mexico katika sherehe za maadhamisho yake ya
pili
tangu achaguliwe,Papa Francis amesema kuwa anahisi kwamba uongozi wake katika
kanisa hilo hautaendelea kwa kipindi kirefu.
Amesema
kuwa hatua ya Benedict kujiuzulu mwaka 2013 ni ya ujasiri na haifai kuchukuliwa
kama ya kipekee.
Papa
Benedict ndiye kiongozi wa kwanza wa kanisa hilo kujiuzulu tangu papa Gregory
wa 12 mwaka 1415.
Papa
Francis anasema kuwa anatamani maisha yake ya kuwa muhubiri na angependelea
kuzuru maeneo kadhaa bila kujulikana..
Kutoka BBC
0 maoni:
Post a Comment