Hatua hiyo inafuatia shinikizo la
kuimarisha afya ya umma na haswa afya ya mama waja wazito.
Sheria hiyo inawadia baada ya kampeini
ya kuwazuia wanawake wajawazito kuingia pahala panapovutiwa sigara jarida la
aGulf News linasema.
Kampeini hiyo inayoendeshwa kwa kutumia
mabango na picha ya mwanamke mjamzito akiambiwa na mwanaye aliyeko tumboni kuwa
''Uamuzi wa kuvata au la ni wako,,,sio wangu''
Mabango hayo yanaeleza kuwa watoto ambao
hawajahitimu miaka 18 na wanawake wajawazito hawaruhusiwi kuvuta shisha au
sigara.
"Kauli hiyo ni ya
serikali wala sio hoja ya kujadiliwa na yeyote '' alisema mkurugenzi wa afya ya
umma wa Dubai bwana Marwan Al Mohammed.
Wamiliki wa vilabu vya burudani
vinavyouza shisha wamekuwa wakilalamikia kutokuwepo kwa sheria zinazoharamisha
wanawake wajawazito kutoingia katika vilabu hivyo.
''Sasa sheria hii inaweka bayana
anayeruhusiwa kisheria kuvuta ima ana pesa au la '' aliongezea kusema.
Mwaka wa 2014 milki hiyo ya kiarabu
ilipitisha sheria kali dhidi ya uvutaji wa sigara ambayo ilipiga marufuku
matangazo ya aina yeyote ya kibiashara ya Sigara.
Vilevile sheria hiyo
ilipiga marufuku uvutaji wa sigara ndani ya gari iwapo mna mtoto mwenye chini
ya umri wa miaka 12.
Aidha sasa kuna sheria inayotoa mwelekeo
ya ni wapi shisha itauzwa na itaruhusiwa kuwepo umbali gani kutoka kwenye
makazi ya watu.
.Kutoka BBC
0 maoni:
Post a Comment