Wakulima katika mji wa Fukushima Japan eneo lililoathirika na kuyeyuka
kwa tanuri ya nyuklia mwaka wa 2011 wamegundua njia mbadala ya kukuza
mazao,,,,wakitumia mchanga bandia!
Katika Jaribio la kwanza katika wilaya ya Ojima mimea 2,000 aina
ya 'ornamental anthurium' ilimea kwa njia nzuri na kuwaridhisha watafiti,
jarida la Asahi Shimbun limeripoti.
Wilaya hiyo ya Ojima iliyoko takriban kilomita 50 kutoka kiwanda
kilichoathirika vibaya zaidi cha nyuklia cha Fukushima Daiichi.
Kiwanda hicho kiliyeyuka
baada ya tetemeko kubwa la ardhi kukumba eneo hilo na kusababisha mafurikoChanzo BBC Swahili
0 maoni:
Post a Comment