Waziri wa afya wa Ubelgiji amesema watu
11 walifariki na wengine 81 kujeruhiwa baada ya milipuko miwili kutokea uwanja
wa ndege wa Zaventem, nje kidogo ya mji wa Brussels.
Kampuni inayosimamia uchukuzi wa treni
Brussels imesema kwamba watu 15 walifariki Maelbeek na wengine 55 kujeruhiwa,
10 kati yao wakijeruhiwa vibaya.
Waziri Mkuu wa Ufaransa Francois
Hollande amelaani mashambulio hayo mjini Brussels na kusema ni kama mashambulio
yaliyolenga bara lote la Ulaya.
Waziri Mkuu wa Ubelgiji Charles Michel
amesema hatua zaidi zimechukuliwa kuimarisha usalama mpakani.
0 maoni:
Post a Comment