MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

TRUMP AYUMBAYUMBA KUHUSU UTOAJI MIMBA

Kura
Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump amebadili msimamo wake muda mfupi baada ya kusema wanawake wanaotoa mimba wanafaa kuadhibiwa, utoaji mimba ukiharamishwa.
Alikuwa ametoa tamko lake katika hafla iliyopeperushwa moja kwa moja na kituo cha runinga cha MSNBC.
Hatua hiyo ilimfanya kushutumiwa vikali.
Lakini muda muda mfupi baadaye, alibadili msimamo wake na kusema ni wahudumu wa afya wanaosaidia wanawake kutoa mimba pekee wanaofaa kuadhibiwa.
Lakini hata baada ya kusema hivyo, alijitetea na kuongeza kuwa: “Msimamo wangu haujabadilika.”
Mgombea huyo anayeongoza katika chama cha Republican anaunga mkono kupigwa marufuku kwa utoaji mimba, lakini kwa kutegemea hali.

Utoaji mimba umekuwa halali nchini Marekani tangu 1973 kufuatia uamuzi wa kihistoria wa Mahakama ya Juu nchini humo.

KUTOKA BBC Swahili
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment